Muheza Hospice Care ni taasisi ya kibinafsi ambayo ilianzishwa mnamo mwaka 2001 kwa lengo la kuhudumia wagojwa wenye maradhi ya kusendeka yaani yasiyotibika kama vile Saratani, kisukari, UKIMWI na kadhalika.
Tiba hii kwa wagonjwa walio na maradhi ya kusendeka huitwa TIBA SHUFAA au palliative care, mfumo wa utoaji tiba ni tofauti na tiba nyingine kwani tiba hii hutolewa na timu maalumu yenye wataalamu mbalimbali kama vile madaktari, manesi, maafisa jamii, viongozi wa dini, viongozi wa kisiasa hususani katika ngazi ya kijiji/kitongoji na wengineo.
tarehe 31 March 2012, Muheza Hospice Care iliazimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake, mgeni wa heshima katika hafla hiyo alikuwa Mhashamu Baba Askofu wa dayosisi ya Tanga ya Kanisa la Kianglikana
Familia ya karolyn na Richard Collins ni moja kati ya waanzilishi wa Muheza Hospice Care, nao walijumuika katika sherehe hizo za miaka kumi.
Ngoma za asili zilikuwepo pia katika kuipamba hafla hiyo.
Maandamano yaliongozwa na Matarumbeta toka kanisa la kilutheri Muheza
Meza kuu: Kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri mheshimiwa kiroboto, akifuaitiwa na Mhashamu askofu, pamoja na mganga Mfawidhi wa Hospitali Teule.
Mganga Mfawidhi akijiandaa kumkaribisha mgeni rasmi
Baadhi ya wageni waalikwa na katikati ni kwaya ya Kanisa la Anglikani-Muheza
Mhashamu Baba askofu akinukuu masuala muhimu yatokanayo
Hata watoto pia walijumuika katika hafla hiyo muhimu.
Kwaya ya kanisa la Angilikani ikitumbuiza
Sehemu ya umati wa wageni waalikwa ambao walhudhuria
Mwenyekiti wa Muheza Hospice Care akiongoza zoezi la kufungua Champagne
Mhashamu askofu akianza kutoa hotuba yake
Keki mahsusi ambayo iliandaliwa kwa hafla hiyo
Mwenyekiti wa Muheza Hospice Care na Karolyn wakijiandaa kukata keki.
Hapa wanajadili mkakati wa kukata keki hiyo
Mwenyekiti anatangaza mkakati huo
Waalikwa toka TPCA na wizara ya Afya walikuepo pia
Baadhi ya wana washiriki wakijiandaa kufungua champagne
Mhashamu Askofu akihutubu katika hafla hiyo
Mhashamu Askofu aliendesha Harambee ya kuchangia watoto waishio mazingira hatarishi ambao wanahudumiwa na Hospice.
Zoezi la harambee likiendelea kwa umakini mkubwa
Baadhi ya washiriki wa hafla hiyo wakiendelea kuchangia
Mhashamu Askofu akitoa zawadi kwa watumishi waliotukuka
Dada Mary Kauki mmoja kati ya waanzilishi akipokea zawadi yake
Huyu nae akijongea jukwaa tayari kupokea zawadi yake
Kwa heshma na taadhima akipokea zawadi yake
Msafara wa maandamano katika maadhimisho hayo
Maandamano yakiendelea
It is a nice support to the underprivileged patients - Pattersen Jeff
ReplyDeleteI am so sad we missed this
ReplyDelete